1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU yaweka mpango wa kupunguza matumizi ya gesi

20 Julai 2022

Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya imepanga kuchapisha mpango wa kulinda usambazaji wa gesi na kuepuka mgogoro wakati wa msimu wa baridi katika Umoja huo kutokana na wasiwasi wa kusitishwa usambazaji wa gesi ya Urusi.

https://p.dw.com/p/4EPHQ
Belgien Brüssel | EU Hauptquartier - Ursula von der Leyen: Vorstellung des Gas Notfallplans
Picha: JOHN THYS/AFP/Getty Images

Katika rasimu ya mpango huo, ambao unaweza kubadilika wakati wowote, Halmashauri Kuu hiyo ya Umoja wa Ulaya imezihimiza nchi wanachama kuendelea na hatua za hiari za kupunguza matumizi ya gesi ili kuepuka mgororo.

Hata hivyo, baadhi ya nchi za Umoja huo zimeonyesha wasiwasi wa kutokea dharura kutokana na usambazaji mdogo wa gesi.

Shirika la kimataifa la kudhibiti nishati ya nyuklia limetoa tahadhari kwamba juhudi za Umoja wa Ulaya za kutafuta gesi mbadala huenda zisifanikiwe kuelekea msimu wa baridi, na kutoa wito kwa nchi hizo kupunguza matumizi yake ya gesi.

Umoja wa Ulaya umejitahidi kuondokana na utegemezi wake wa nishati ya Urusi, huku mwaka jana umoja huo ukiagiza asilimia 40 ya gesi yake kutoka Moscow.