1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Urusi: Mafuta hayataathiri mashambulizi nchini Ukraine

5 Desemba 2022

Ikulu ya Urusi Kremlin imesema leo kuwa azimio la mataifa ya magharibi kuweka ukomo wa bei kwa mafuta ya Urusi halitaathiri kampeni ya kijeshi ya Moscow nchini Ukraine.

https://p.dw.com/p/4KUka
Der russische Pressesprecher Dmitry Peskov
Picha: Elena Palm/ZUMAPRESS.com/picture alliance

Msemaji wa ikulu ya Kremlin Dmitry Peskov  amewaambia waandishi habari kwamba uchumi wa Urusi una uwezo kamili wa kumudu gharama na mahitaji yote ya operesheni zake katika vita vinanyoendelea nchini Ukraine.

Kwa mara nyingine Peskov amesisitiza pia kuwa Urusi haikubaliani na uamuzi huo wa kuwekwa ukomo wa bei kwa mafuta yake na ameapa kwamba Moscow itajibu hatua hiyo ya nchi magharibi.

Umoja wa Ulaya, kundi la mataifa yaliyostawi kiuchumi la G7 na Australia yalitangaza mwishoni mwa juma lililopita makubaliano ya kununua mafuta ya Urusi kwa bei isiyopindukia dola 60 kwa pipa, uamuzi unaolenga kuhujumu mapato ya Urusi kwenye sekta yake ya nishati.