1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

UN yaonya watu laki nane wapo katika hatari Sudan

20 Aprili 2024

Umoja wa Mataifa Umeonya takriban watu 800,000 nchini Sudan wapo katika "hatari kubwa" huku ghasia zinazozidi kuongezeka zinatishia "kuchochea mapigano ya umwagaji damu" kati ya jamii mbalimba katika eneo la Darfur."

https://p.dw.com/p/4f013
Umoja wa Mataifa | Mkuu wa masuala ya kisiasa Rosemary DiCarlo
Mkuu wa masuala ya kisiasa wa Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo Picha: Eskinder Debebe/Xinhua News Agency/picture alliance

Mkuu wa masuala ya kisiasa wa Umoja wa Mataifa Rosemary DiCarlo ameliambia Baraza la Usalama kwamba, mapigano kati ya wanamgambo wa RSF na jeshi la Sudan yanakaribia mji mkuu wa jimbo la Darful wa El Fasher.

Umoja huo umoengeza kuwa karibu watu milioni 25, ikiwa ni takriban nusu ya wakaazi wa Sudan wanahitaji msaada wa kibinadamu huku wengine milioni 8 wakiyakimbia makaazi yao.

Mashirika ya kiraia na Umoja wa Mataifa mwishoni mwa mwezi uliopita, yalisema hatua za haraka zinahitajika ili "kuzuia kuongezeka kwa vifo" kutokana na njaa.

Soma pia:Euro bilioni mbili zapatikana kwa ajili ya kuisaidia Sudan

Siku ya Jumatatu wafadhili waliahidi zaidi ya dola bilioni 2 kwa ajili ya Sudan iliokubwa na vita kwa mwaka mmoja sasa.