1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kampeni ya kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake yaanza

25 Novemba 2022

Wakati ulimwengu ukianza siku 16 za kutokomeza ukatili wa kijinsia", wanawake wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanahisi kwamba vita kwenye eneo hilo vinachangia pakubwa kuharibu zaidi hali ya mambo.

https://p.dw.com/p/4K5CK
Afrika DR Kongo Kayembe Camp
Picha: GUERCHOM NDEBO AFP via Getty Images

Wanawake kutoka mashirika mbalimbali ya utetezi wa haki za wanawake wamekutana hapa Bukavu kutahmini mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia ya zaidi ya muongo mmoja sasa.

Jinsi wanawake walivyogeuzwa shabaha ya wapiganaji Kongo

Kwenye mkutano wao huu, wanasema ingawa unyanyasaji dhidi ya wanawake umepunguwa katika siku za karibuni kutokana na uhamasishaji, lakini vita vya mara kwa mara mashariki ya Kongo vinaweza kuirudisha hali kubwa mbaya kuliko ilivyokuwa.

Licha ya kupungua kwa visa vya ubakaji, wanawake hawa wamegundua kuwa kwa sasa ni ukatili wa nyumbani unaofanyika kwa kiwango cha juu zaidi, wanawake wengi wakiwa waathirika katika familia zao.

Wanawake wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wahisi vita vinachangia pakubwa kuharibu zaidi hali ya mambo.
Wanawake wa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wahisi vita vinachangia pakubwa kuharibu zaidi hali ya mambo.Picha: Alexis Huguet/AFP/Getty Images

Mamlaka ya Kivu Kusini imesema athari za janga la korona, hali ya ukosefu wa ajira na pia mabadiliko ya tabianchi vimechangia pakubwa katika ongezeko la aina hiyo ya ukatili wa nyumbani.

Wanawake Afghanistan waandamana mjini Kabul

Lakini vil evile, baadhi ya mashirika ya kiraia yamechukua fursa ya kampeni hii kwa kulaumu mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yanayotangaza takwimu zisizokuwa sahihi kuhusiana na visa vya ubakaji mashariki ya Kongo.

Pia, wanawake wa Kivu Kusini wamechukua fursa hii kuunga mkono mikakati ya wagombea wanawake kwenye uchaguzi unaopangwa mwakani hapa Kongo.

Mwandishi: Mitima Delachance/DW Bukavu