1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hakuna tuzo za Ballon d'Or mwaka huu kutokana na COVID-19

Sekione Kitojo
20 Julai 2020

Tuzo za mchezaji  bora wa mwaka maarufu kama Ballon d'Or hazitakuwapo mwaka huu kwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa mnamo  mwaka 1956 kwasababu ya  janga la virusi vya corona.

https://p.dw.com/p/3fbk1
Fußball Ballon d'Or 2019 | Lionel Messi
Lionel Messi ndio mshindi wa mwisho wa Ballon d'Or, hadi mwaka 2021Picha: Reuters/C. Hartmann

Watayarishaji  'Jarida la  michezo la  Ufaransa',  wamesema  leo Jumatatu (20.07.2020) kuwa  kutomalizika  kwa  baadhi  ya  ligi pamoja  na  kuahirishwa kwa  michuano  ya  Euro 2020  pamoja  na Copa America hakukuweza  kuruhusu  upigaji  kura wa  haki.

Nadine Keßler
Mteule wa tuzo ya mchezaji bora kutoka Ujerumani mwaka 2014 Nadine KesslerPicha: Getty Images/P. Schmidli

"Matukio  ambayo  ni  ya  kipekee, maamuzi  ya  kipekee,"   taarifa ya  France Football imesema. "Mwaka  kama  huu  wa  aina  yake hauwezi , na  haupaswi , kuwa  kama  mwaka  wa  kawaida."

Ballon d'Or   hutolewa  katika  kura  inayopigwa  miongoni  mwa waandishi  wa  habari  za  michezo. Kati ya  mwaka  2010  na  2015 France Football  iliunganisha   nguvu  zake  na  shirikisho linaloangalia  mchezo  wa  kandanda  FIFA  pamoja  na  tuzo  hiyo lakini makundi hayo  mawili  yalijitenga kutoa  zawadi  zao  tena mwaka  2016.

Paris Ballon d'Or Verleihung Modric
Mwaka 2018 tuzo hiyo ilikwenda kwa Luka ModricPicha: Reuters/B. Tessier

Lionel Messi  wa  Barcelona ni mshindi mara nyingi  zaidi  akiwa  na tuzo sita.

France Football imesema  kuwa  Ballon d'Or  itarejea  tena  mwaka 2021.