1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Guterres ataka uchaguzi Sudan Kusini kufanyika

18 Aprili 2024

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amevitaka vyama vyote vya siasa nchini Sudan Kusini kuchukua "hatua za haraka" kuruhusu uchaguzi uliocheleweshwa kwa muda mrefu kufanyika mwishoni mwa mwaka huu.

https://p.dw.com/p/4eupU
Antonio Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres.Picha: Robertson S. Henry/REUTERS

Katika ripoti yake iliyochapishwa siku ya Jumatano (Oktoba 17), Guterres aliandika kwamba, kwa maoni yake, vyama lazima vijitolee kuchukua hatua za haraka kupata taasisi muhimu za kuendesha uchaguzi huru wa amani, wa haki na wa kuaminika.

Soma zaidi: Juhudi za amani Sudan Kusini zasambaratika tena

Sudan Kusini haijafanya uchaguzi tangu ilipojinyakulia uhuru wake kutoka kwa Sudan mwaka 2011 na taifa hilo linakumbwa na ghasia, umaskini na majanga ya asili.

Mipango ya uchaguzi imevurugwa na mabishano makali kati ya Rais Salva Kiir na hasimu wake mkuu, Makamu wa Rais Riek Machar.

Waangalizi wa kimataifa wana mashaka iwapo muda mpya uliowekwa kufanyika uchaguzi wa Disemba mwaka huu utaheshimiwa, kwani Kiir na Machar bado hawajafikia muafaka wa kuandaa uchaguzi huo.