1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mugabe, Tsvangirai uwanjani

14 Julai 2013

Mahasimu wa kisiasa nchini Zimbabwe, Rais Robert Mugabe na Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai wamenadi sera zao kwa malengo ya kulikwamua taifa hilo kiuchumi, ikiwa ni jitihada za kuwavutia wapiga kura kabla ya Machi 31.

https://p.dw.com/p/197Q4
Supporters cheer Zimbabwean President Robert Mugabe as he arrives to launch his ruling ZANU PF party's election manifesto in the capital Harare July 5, 2013. Zimbabwe's Constitutional Court rejected a series of government appeals on Thursday to delay a July 31 general election in order to allow more time for reform of the security forces and state media. REUTERS/Philimon Bulawayo (ZIMBABWE - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Rais Robert MugabePicha: Reuters

Kwa mujibu wa tathmi ya shirika la habari la Ufaransa AFP mahasimu hao "walirindima", mwishoni jumamosi ikiwa zimebaki wiki si zaidi ya tatu kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa taifa hilo, unaotarajiwa kufikisha kikomo serikali yao ya mizengwe iliyolazimishwa kuundwa kutokana na uchaguzi wenye vurugu wa 2008.

Akizungumza katika kampeni yake katika taifa hilo lenye utajiri mkubwa wa madini ya almas kwa upande wa mashariki, Tschangirai alisema " Chaguo ni rahisi sana, ni kati ya serikali iliyoshindwa kwa zaidi ya miaka 33 na ahadi mpya ambazo ziko wazi kabisa" Kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 61 alizungumza katika mji wa Mutare akimtolea mfano rais Mugabe kuwa mwenye kutaka kuhodhi madaraka.

Mugabe na sera za uzawa

Mugabe mwenye umri wa miaka 89, akiwa amevalia kanzu nyeupe huku ameshika biblia mkononi alijitokeza mbele ya maelfu ya wafuasi wake waliokusanyika katika eneo la kanisa moja huko mjini Marange, umbali wa kilometa 200, mashariki mwa mji mkuu Harare. Akinukuliwa na AFP kiongozi huyo mkongwe barani Afrika alisema"Tulifanya makosa 2008 kumchagua mtu ambae anapenda Wazungu. Kumpigia kura mtu ambae anataka kuwarejesha wazungu na ambae anafikiri haiwezekani kuwepo kwa maendeleo nchini Zimbabwe bila kuhusishwa watu hao" Alisema rais Mugabe.

Supporters cheer Zimbabwean President Robert Mugabe as he arrives to launch his ruling ZANU PF party's election manifesto in the capital Harare July 5, 2013. Zimbabwe's Constitutional Court rejected a series of government appeals on Thursday to delay a July 31 general election in order to allow more time for reform of the security forces and state media. REUTERS/Philimon Bulawayo (ZIMBABWE - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Wafuasi wa Robert MugabePicha: Reuters

Katika kunadi sera zake kiongozi huyo mkongwe alilenga masuala ya uzawa, au sera za uzawa na kuwawezesha watu weusi akisema kwamba Zimbabwe lazima imiliki sehemu kubwa ya rasilimimali yake. Kwa upande wake Tsvangirai ameahidi kurekebisha uchumi, kufufua viwanda na kuvutia uwekezaji kwa lengo la kupanua wigo wa ajira kwa vijana nchini humo.

Almas kwa Wazimbabwe wote

Akizungumza mbele ya maelfu ya wafuasi waliovaa fulana nyekundu zenye picha yake. Tsvangirai ameahidi kufanikisha uwazi katika uchimbaji wa madini ya almas. Nikimunukuu kiongozi huyo wa upinzani hapa alisema " Wapi zinapokwenda fedha za almas? Tunafahamu tukipata fedha zote kutoka katika madini hayo tunaweza kuunda ajira mpya laki moja. Alisema katika mkutano wake wa kampeni uliyofanyika katika uwanja wa Mutare, uliyopo kilometa 250 mashariki mwa Zimbabwe.

Zimbabwe opposition Movement For Democratic Change (MDC) leader Morgan Tsvangirai speaks at the launch of his party's election campaign in Marondera, about 70 km (43 miles) east of Harare, July 7, 2013. Tsvangirai, launching his third campaign to unseat veteran President Robert Mugabe, said nothing had been achieved to ensure a fairer vote but even God now wanted Mugabe to go. REUTERS/Philimon Bulawayo (ZIMBABWE - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Mgombea urais Zimbabwe Morgan TsvangiraiPicha: Reuters

Aliongeza kusema kama mapato yote kutoka katika madini hayo yangefika moja kwa moja katika mikono ya serikali wangaliweza kulia walimu na wanajeshi na sio kama ilivyo sasa ambapo mapato hayo yanawanufaisha watu wachache. Kama atapewa ridhaa ya Wazimbabwe kuongoza taifa hilo Tsvangirai ameahidi kupitia upya mikataba yote katika sekta ya madini kwa kuwa ya sasa inatoa mianya ya kuendelea kwa vitendo vya rushwa.

Aidha katika kampeni yake rais Robert Mugabe amepinga ndoa za jinsia moja kuwa zinakwenda kinyume na utamaduni wa Afrika na kuikosoa vikali kauli ya rais Obama barani wakati alipozulu Afrika kuhimiza waafrika kuheshimu haki za mashoga. Mugabe alisisitza kauli yake hiyo kwa kusema ndoa ni ya mwanamke na mwanaume ambapo matunda yake ni kuzaliwa watoto.

Katika uchaguzi uliyopita Zimbabwe iligubikwa na visa vya umwagikaji damu. Tsvangirai alijiondoa katika kinyanganyiro hicho pamoja na cha mwaka 2008 pamoja na kuibuka na ushindi katika duru ya kwanza. Uchaguzi wa mwezi huu unatajwa kuwa wenye kuweza kuifikisha serikali ya mseto nchini humo ambayo imesababisha kudidimia kwa uchumi.

Mwandishi: Sudi Mnette AFP
Mhariri: Sekione Kitojo.