1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Moyo afafanua kilichotokea uchaguzi wa Zanzibar 2010

Josephat Charo23 Oktoba 2014

Mwanasiasa mkongwe nchini Tanzania, Hassan Nassor Moyo, anaamini ushawishi wake kwa kiongozi wa CUF, Seif Sharif Hamad, ulichangia kuinusuru Zanzibar isitumbukie kwenye umwagikaji damu mwaka 2010.

https://p.dw.com/p/1DaBP
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na aliyekuwa mgombea urais kwenye uchaguzi wa 2010, Maalim Seif Sharif Hamad.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar na aliyekuwa mgombea urais kwenye uchaguzi wa 2010, Maalim Seif Sharif Hamad.Picha: DW/M.Khelef

Kufuatia taarifa zilizochapishwa na vyombo vya habari vya Tanzania juu ya nafasi ya Mzee Moyo kwenye uchaguzi wa Zanzibar mwaka 2010, Josephat Charo alizungumza na mwanasiasa huyo ambaye alikuwa mjumbe kwenye Baraza la kwanza la Mapinduzi la Zanzibar chini ya Marehemu Abeid Karume, Waziri wa Sheria wa Muungano, Waziri wa Elimu wa Zanzibar na sasa Mwenyekiti wa Kamati ya Maridhiano, juu ya mchango wake huo, hasa kwa kuwa vyombo vya habari viliandika chama tawala cha CCM kilikuwa tayari kwa lolote lakini sio kutangazwa mgombea wa kilichokuwa chama cha upinzani, CUF, kama mshindi wa urais kwenye uchaguzi huo.

Katika mahojiano haya, Mzee Moyo kwanza anaelezea vipi aliweza kumshawishi mgombea wa CUF, Seif Sharif Hamad, akubali ushindi wa mpinzani wake mgombea wa CCM na rais wa sasa wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein. Kusikiliza mahojiano kamili, tafadhali bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini

Mwandishi: Josephat Charo
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman