1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kiwakumbacho walemavu wa ngozi si mauaji pekee

Eric Ponda31 Machi 2015

Ingawa si visa vingi vya utekaji nyara watu wenye ulemavu wa ngozi vinavyoripotiwa katika Pwani ya Kenya, tatizo kubwa linalowakera walemavu hao ni ubaguzi, kudhalilishwa na kujihisi kutengwa.

https://p.dw.com/p/1Ezv8
Mwanamuziki mwenye ulemabu wa ngozi nchini Kenya, Kamanu M'tuamwari.
Mwanamuziki mwenye ulemabu wa ngozi nchini Kenya, Kamanu M'tuamwari.Picha: DW/R. Kyama

Hali hiyo imewalazimisha wengi kutegemea misaada kutoka kwa wahisani ikiwa ni pamoja sekta ya utalii, inayotoa sehemu kubwa ya mchango wa mafuta ya kuikinga ngozi dhidi miale ya jua.

Hata hivyo, kuzorota kwa sekta ya utalii nchini humo sasa kunaathiri pakubwa usambazaji wa misaada hiyo na kuwafanya baadhi yao wazigeukie kazi zinazohataraisha zaidi afya na usalama wao.

Msikilize Eric Ponda akiripoti kutoka Mombasa kwa kubonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.

Mhariri: Mohammed Khelef