1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hapo zamani za Kale – Hadithi kuhusu Afrika

27 Aprili 2011

Yaaminika bara la Afrika ndilo chimbuko la mwanadamu. Bara hili limekuwa makaazi ya falme nyingi na pia lililopoteza watu wake wengi kupitia biashara ya watumwa.

https://p.dw.com/p/MBAd
Hadithi kuhusu AfrikaPicha: LAI F

Kwa upande mwengine tunaweza kusema asili ya mwanadamu ni Afrika. Hapa ndipo mwanadamu wa kwanza duniani yaamika aliishi. Miaka mingi baadaye, utawala wa kifalme ulianza kukita mizizi, kusambaa na hata kutukuzwa katika bara hili. Historia ya Afrika pia inatupa kumbukumbu ya nyakati za giza kama vile biashara ya watumwa, na utawala wa kikoloni uliotekelezwa na Wazungu.

Hebu sasa tuanze safari yetu kupekua historia ya Bara hili la Afrika na jinsi historia hii inavyochangia maisha ya sasa barani humu. Kama wasemavyo wahenga, “Ili kupata kujua unakokwenda ni lazima ujue unakotoka.”

Hata hivyo haya yasikujalishe kwani hayamo kwenye maandiko na kumbukumbu ya vitabu vya historia. Safari yetu kuhusu historia ya karne nyingi zilizopita barani Afrika, inazunguka katika maisha ya msichana mmoja kwa jina Julie, ambaye pamoja na bibi yake, wanafanya utafiti kuhusu historia ya bara hili.

Vipindi vya "Learning by Ear - Noa bongo Jenga Maisha yako" vinasikika katika lugha sita: Kiingereza, Kifaransa, Kiswahili, Hausa, Kireno na Amharic. Na vinafadhiliwa na wizara ya mambo ya nchi za kigeni ya Ujerumani.