1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Hakuna mshindi wa wazi Merkel na Steinbrück

2 Septemba 2013

Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, na mgombea wa kiti cha ukansela wa chama cha SPD, Peer Steinbrück, walipambana katika mjadala pekee jana(01.09.2013) wa televisheni kabla ya uchaguzi mkuu, Septemba 22.

https://p.dw.com/p/19Zx3
German Chancellor Angela Merkel shakes hands with her challenger, the top candidate in the upcoming German general elections of the Social Democratic Party (SPD), Peer Steinbrueck, during their TV duel in Berlin, September 1, 2013. German voters will take to the polls in a general election on September 22. REUTERS/ARD/Max Kohr/Pool (GERMANY - Tags: POLITICS ELECTIONS) FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. MANDATORY CREDIT. ATTENTION EDITORS: PICTURE TO BE USED ONLY IN RELATION TO THE TV DEBATE
Wagombea wa kiti cha ukansela Angela Merkelwa CDU na Peer Steinbrück wa SPDPicha: Reuters

Maoni ya wapiga kura yaligawika kuhusiana na nani ameshinda mjadala huo.

Baadhi ya wachambuzi wamesema kuwa mjadala huo umemfaidia zaidi Peer Steinbrück, kwa kuwa anakosa kuanikwa kitaifa katika masuala mbali mbali ambapo Merkel amekuwa akionekana mara kwa mara akiyashughulikia katika miaka minane ya utawala wake.

People watch a TV duel of German Chancellor Angela Merkel of the Christian Democratic Union (CDU) with her challenger, the top candidate of the Social Democratic Party (SPD) in the upcoming German general elections Peer Steinbrueck, in Berlin, September 1, 2013. German voters will take to the polls in a general election on September 22. REUTERS/Fabrizio Bensch (GERMANY - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Kansela Angela MerkelPicha: Reuters

Mataifa dhaifu

Kuhusiana na msaada kwa mataifa dhaifu ya eneo la euro , Merkel , ambaye msimamo wake imara umesaidia kuwavuta wapiga kura wahafidhina wa Ujerumani, amekataa kutamka iwapo Ugiriki itahitaji kiasi gani kingine cha mpango mwingine wa tatu wa uokozi wa uchumi wake mwakani.

"Hakuna mtu ajuaye kwa hakika mambo nchini Ugiriki yanavyoendelea. Ni jukumu langu kama kansela kuona kwamba mbinyo wa kuleta mageuzi dhidi ya Ugiriki hausiti. Inawezekana kuwa kutahitajika mpango mwingine wa uokozi kwa Ugiriki." amesema kansela Merkel. Kansela huyo vile vile ametetea maamuzi ya serikali yake na kusema chama chake kina uwezo wa kushughulikia mambo".

"Tumeonesha kuwa tunaweza , na katika wakati mgumu kabisa , ambapo wakati fulani tulipata matatizo makubwa ya mzozo wa kifedha katika bara la Ulaya, Ujerumani iliendelea kuwa imara, Ujerumani ilikuwa injini ya ukuaji wa uchumi, Ujerumani ilikuwa mhimili wa uthabiti, na njia hii ndio ninayotaka kuiendeleza".

People watch a TV duel of the top candidate of the Social Democratic Party (SPD) in the upcoming German general elections Peer Steinbrueck with German Chancellor Angela Merkel of the Christian Democratic Union (CDU) in Berlin, September 1, 2013. German voters will take to the polls in a general election on September 22. REUTERS/Fabrizio Bensch (GERMANY - Tags: POLITICS ELECTIONS)
Mgombea wa SPD Peer SteinbrückPicha: Reuters

Steinbrück amehimiza kuwepo na huruma zaidi kwa mataifa dhaifu ya eneo la euro, akisema kuwa "Huwezi kuwashikia kirungu Wagiriki; unahitaji kuwapa nafasi kidogo ya kuishi."

"Ninafarijika kuona nchi ikipata mafanikio baada ya kuporomoka. Ninafarijika kuiona nchi ikiwa iko tena imara, kwa kuwa ni haki yao kuuweka sawa uchumi wao na kuwekeza katika jamii yake pia. Nataka kuiona nchi ambayo mikono yake yote inafanya kazi".

Ambeza Steinbrück

Merkel amembeza Steinbrück , ambaye alikuwa waziri wake wa fedha chini ya serikali ya mseto iliyoundwa kwa pamoja na vyama hivyo vikuu vya kisiasa mwaka 2005 hadi 2009, kwa kile alichokisema wakati huo kuwa hatawahi tena kufanya kazi chini yake, lakini ametoa nafasi iwapo atahitajika kukiomba chama hicho cha SPD kurejea muungano wa aina hiyo iwapo hatakuwa na chaguo lingine.

''Nafikiri ni kichekesho sababu za SPD za kukataa kuunda serikali pamoja na chama cha CDU. Hakuna mtu anayetafuta hali hiyo. Hii ni hali mbaya kwa chama changu pia'', amesema kansela Merkel katika mjadala huo mjini Berlin, na kuongeza kuwa kilicho muhimu zaidi ni taifa.

Bildnummer: 60414525 Datum: 30.08.2013 Copyright: imago/Xinhua (130830) -- BERLIN, Aug. 30, 2013 (Xinhua) -- (From L to R) Stefan Raab, Anne Will, Maybrit Illner and Peter Kloeppel, TV presenters of a TV debate between German Chancellor Angela Merkel and chancellor candidate of Social Democratic Party (SPD) Peer Steinbrueck, pose for photos in a television studio where the debate will be presented in Berlin, Germany, Aug. 30, 2013. Merkel will face her opposition challenger Steinbrueck in their only TV debate here on Sunday for Germany s upcoming state and general elections which will fall on Sept. 22, 2013. (Xinhua/Zhang Fan) GERMANY-BERLIN-POLITICS-ELECTIONS-TV DEBATE PUBLICATIONxNOTxINxCHN People Entertainment x0x xkg 2013 quer premiumd 60414525 Date 30 08 2013 Copyright Imago XINHUA Berlin Aug 30 2013 XINHUA from l to r Stefan Raab Anne will Maybrit Illner and Peter Kloeppel TV Presenters of a TV Debate between German Chancellor Angela Merkel and Chancellor Candidate of Social Democratic Party SPD Peer Steinbrueck Pose for Photos in a Television Studio Where The Debate will Be presented in Berlin Germany Aug 30 2013 Merkel will Face her Opposition CHALLENGER Steinbrueck in their Only TV Debate Here ON Sunday for Germany S upcoming State and General Elections Which will Case ON Sept 22 2013 XINHUA Zhang supporter Germany Berlin POLITICS Elections TV Debate PUBLICATIONxNOTxINxCHN Celebrities Entertainment x0x xkg 2013 horizontal premiumd
Kikosi cha waendesha mjadala kutoka vyombo vya habariPicha: imago stock&people

Vituo vinne vikubwa vya televisheni ambavyo vimerusha mjadala huo wa dakika 90 wameona maoni ya watazamaji kuwa yamegawanyika kuhusu nani ameshinda.

Maoni yaliyochukuliwa na kituo cha taifa cha ZDF yamempa ushindi Merkel wakati kituo cha kwanza cha taifa ARD kimempa ushindi Steinbrück.

Mwandishi : Wolfgang Dick / ZR / Sekione Kitojo

Mhariri: Gakuba Daniel