Tanzania imeanzisha mchakato wa kuwatambua na kuwasajili raia na wasiokuwa raia katika nchi hiyo ili baadae kutoa vitambulisho vya utaifa.
Kwa mujibu wa mamlaka ya vitambulisho nchini humo ni kwamba vitambulisho vya utaifa vinatazamiwa kuanza kutolewa mwishoni mwa mwaka huu.
Othman Miraji alizungumza kwa njia ya simu na mkurugenzi mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya taifa, Dickson Mwaimu, juu ya zoezi hilo. Lina madhumuni gani hasa?
Mahojianio/Othman Miraji/Dickson Mwaimu
Mpitiaji:M.Abdul-Rahman