Wengi husema kuwa Vyombo vya habari hutoa taarifa za mambo mabaya tu kuhusu Afrika, lakini kwa msaada wako msikilizaji hili tunaweza kulibadili..
Kwa hiyo Idhaa ya kiswahili ya DW inakupa nafasi ya
Kututumia taarifa njema, yakiwa ni Maelezo marefu juu ya Maendeleo na watu walio na Ushawishi wa kuleta mabadiliko na mafanikio katika jamii nchini mwako…….nasi tutautumia mchango wako kwenye mfululizo wa matangazo yetu.
Iwapo taarifa yako itakuwa miongoni mwa zilizo bora zaidi, basi huenda ukawa mshindi wa Simu ya mkononi , miongoni mwa zawadi nyingine tele.
Unaweza kutuma mchango wako kwa kutumia anuani ifuatayo:Deutsche Welle´, Idhaa ya Kiswahili, 53110 Bonn, Ujerumani .
Au Sanduku la Posta 70087 Dar es Salam Tanzania
Na Sanduku la Posta 47504 00100 Nairobi Kenya.
Au pia unaweza kututumia barua pepe kupitia
Kiswahili@dw-world.de
Tarehe ya mwisho ni Agosti mosi mwaka huu !!!