1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Blatter: ubaguzi lazima uangamizwe

2 Machi 2015

Rais wa FIFA Sepp Blatter ameleezea wasiwasi wake kuhusiana na ripoti inayoonesha kiwango cha tatizo la ubaguzi wa rangi katika kandanda la Urusi, kabla ya Kombe la Dunia la mwaka wa 2018

https://p.dw.com/p/1EjxJ
Joseph Blatter Fifa 31.01.2015
Picha: Ryan Pierse/Getty Images

Blatter ameonya kuwa “lazima hatua kadhaa zichukuliwe” kama matukio ya utovu wa nidhamu katika kandanda hayataangamizwa.

Ripoti iliyotolewa na Fare network, shirika la kupambana na ubaguzi katika kandanda, na Kituo cha SOVA chenye makao yake mjini Moscow, inaonyesha kuwa Urusi imesakamwa na utamaduni wa mashabiki kuwa na tabia za kibaguzi na hisia kali.

Blatter alizungumza mwezi Julai mwaka jana na Rais wa Urusi Vladmir Putin akimtaka alipatie kipau mbele suala la kupambana na matukio ya kibaguzi, lakini visa vya uovu huo vinaendelea kutoa picha mbaya kwa nchi hiyo mwenyeji wa Kombe la Dunia 2018, pamoja na mechi za Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Mwandishi: Bruce Amani/AFP/reuters
Mhariri: Mohammed Khelef