1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Balaa la Wakimbizi wa Kiafrika Mediterania

12 Mei 2015

Wakimbizi takriban 100 ambao walisema walikuwa baharini kwa siku 12 waliokolewa Jumatano wiki ya kwanza ya mwezi Mei mwaka 2015 na walinzi wa pwani wa Italia.

https://p.dw.com/p/1FOo3
Symbolbild Flüchtlinge Mittelmeer EU
Picha: Reuters/I. Zitouny

Umoja wa Mataifa Jumatatu (11.05.2015) uliarifiwa kuhusu janga la wahamiaji katika bahari ya Mediterenia na mapendekezo yatakayowalenga wafanyabisahara haramu ya kusafirisha binadamu wanaozidi kuuchochea mzozo huo.

Kuokolewa kwa watu hao, thuluthi moja kati yao wakiwa wanawake, ambao watatu walikuwa wajawazito, ni tukio la hivi karibuni la kuokolewa maelfu ya wakimbizi wanaojaribu kuingia Ulaya kutumia boti za walanguzi. Wengi wao wamekuwa wakianzia safari yao kutoka pwani ya Libya, ambako wafanyabiashara ya kusafirisha binadamu wamekuwa wakiendesha shughuli zao bila hofu ya kukamatwa wala kuchukuliwa hatua yoyote kisheria na wakiutumia mzozo wa kisiasa na machafuko yanayoendelea nchini humo.

Katika kipindi chetu cha Maoni Mbele ya Meza ya Duara leo tunajadili suala la wakimbizi wa kiafrika kukimbia nchi zao na kujaribu kuingia Ulaya kutafuta maisha mazuri na maafa yanayoshuhudiwa katika bahari ya Mediterania na katika pwani ya Italia. Mwenyekiti ni Josephat Charo.

Kusikiliza kipindi bonyeza alama ya spika hapo chini.

Mwandishi:Josephat Charo

Mhariri:Daniel Gakuba